JE, ITAKUWA LINI?

Tafadhali usizielewe vibaya aya hizo hapo juu. Ingwaje waovu wataunguzwa kabisa hapa duniani, dunia iliumbwa ili iweze kurithiwa milele. Mungu ataisafisha hii dunia kwa moto na kisha ataitakasa kwa kuifanya upya kwa misingi ile ambayo iliumbiwa kwayo toka mwanzo.

Baada ya kuangamiwa kwao waovu, Mungu atayafanya mambo yote kuwa mapya kwa kuifanya misingi ya dunia na kuanzisha utawala wake wa milele.

 

Mhubiri 1:4 Kizazi huenda, kizazi huja, nayo dunia hudumu daima.

Isaya 45:18 Maana BWANA, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine.

RUDI KWENYE KURASA KUU