JE, NANI ATAPASWA KUFA HII MAUTI YA PILI?

Wale watakao hukumiwa kuingia kwenye hukumu mauti hii ya pili ni wale wote ambao hawakumkubali Yesu Kristo na kuzishika amri zake. Kama walikataa kuukubali ukweli wa kwamba alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zao na iwapo kama hawakubatizwa (tendo linalouonyesha ulimwengu toba yao), kwa hiyo, majina yao hayataonekana kwenye kitabu cha uzima. Watatupwa kwenye ziwa la moto kukifuatiwa na mauti na kuzimuni (kaburini) na hawataishi tena kwa kuwa watafanyika kuwa majivu yakanyagwayo na nyayo za miguu ya watakatifu.

Wakati hali hii ikitokea hakutakuweko na kifo tena na wale watakao salia wataishi maisha ya milele.

RUDI KWENYE KURASA KUU