JE, KWA NINI ILIMPASA KRISTO KUFA?

Je, ni kwa nini mtu, safi na asiye na dhambi, afe kifo kama hiki cha kutisha msalabani?

Wakati mwanadamu alipofanya dhambi kwenye Bustani ya Eden, alilazimika kufa kama ni hukumu yake kwa kosa la kula tunda lililo katazwa. mauti hii ingekuwa ni ya milele kama Mungu asingeweka njia ya kuiepuka kwa kumtumwa Mwana wake mpendwa na wa pekee ili afe kwa ajili yetu. Damu ni uhai wa mwili, kwa hiyo basi, tendo la kumwaga damu husababisha kifo. Kwa hiyo, pasipo kumwagwa kwa damu hakuwezekani kuwepo kwa ondoleo (ama msamaha) wa dhambi. Ni Kristo tu aliye paswa kufa mara moja ili atuokoe wanadamu wote, sawa na vile ilivyotokea kwamba kwa kupitia dhambi za mtu mmoja mauti iliweza kumpata kila mwenye mwili.

Kristo alikufa ili atuokoe kutoka katika mauti ya milele iwapo tu kama tukiamwani kwa kiasi cha kuzishika amri zake hadi mwisho.

RUDI KWENYE KURASA KUU