JE, MWANADAMU ANA MAJUKUMU GANI?

 

Watati Mungu alipomuumba Mwanadamu alimpa uhuru wa kufanya maamuzi kati ya kumtumikia yeye (Mungu) au kumtumikia Shetani. Uamuzi wa kuchagua kati ya uzima na mauti.

Iwapo kama mwanadamu itachagua kumtumikia Mungu aliye hai wa pekee na wa kweli, basi atapata baraka nyingi zisizoweza kufananishwa, lakini kama utaamua kutumikia uovu basi kutakuwa na laana ya mwisho ya mauti ambayo haina kurudi tena.

Basi ni wajibu wa mwanadamu kumchagua Mungu huyu wa pekee na wa kweli, Yehova, na kuzishika amri na sheria zake zote.

Basi, ni juu yetu kuamua kuchagua kumfuata Yehova kwa kujitahidi kuwa wakamilifu katika utumshi wetu kwake. Tunapaswa kujitahidi kuzifuata amri na njia zake zote kwa siku zetu zote zilizobakia za maisha yetu.

Ni kazi yetu pia kuishi maisha yetu kwa njia kama hii ambayo kwayo tutafanyika kuwa ni mfano mzuri kwa wengine. Tunapaswa kila wakati kuwa tayari kuwa na jibu la kwa nini, ni vipi na ni kitu gani tunachokiamini.

RUDI KWENYE KURASA KUU