Je, Kwa nini Mwanadamu aliwekwa Duniani?

Mwanadamu aliwekwa hapa duniani na kupewa uhuru wa kuchagua kati ya kumtumikia Yehova au kumkataa. Mwanadamu alipewa uhuru wa kuchagua, ambao ulipelekea matokeo ya kuchagua uzima ama mauti. Mwanadamu hakupewa hiyari ya kuchagua kuumbwa kwake kwa hiyo hii ilifanyika kwa kupewa kwake uhuru wa kuchagua kuwepo kwake (yaani uzima) ama asiishi (yaani kifo, ambayo imefafanuliwa kwenye swali la pili). Mwanadamu alipewa ulimwengu wote na kila kiumbe chenye uhai ili viwe chini ya utawala ama uangalizi wake.

 

Mwanadamu alipewa kazi au jukumu la kuvitunza ama kuviangalia na kumtumikia Yehova peke yake na sio kuitumikia miungu mingine iwayo yote ile. Hivyo basi, hawakuweza kujishughulisha na aina iwayo yote ile ya mingu ya kipagani ama tamaa ziwazo zote zilizoko hapa duniani.

RUDI KWENYE KURASA KUU